
Waziri wa Fedha wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amewasili Banjul, Gambia, kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa African Caucus wa 2026, unaotarajiwa kuanza tarehe 6 Julai 2026. Mkutano huu utawaleta pamoja viongozi wa Afrika, watunga sera, wataalamu wa fedha, washirika wa maendeleo, na wawakilishi wa taasisi za kimataifa. Mhe. Omar alipokelewa na Balozi Selestine Kakele wa Tanzania nchini Gambia.