
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewataka Watanzania kujenga utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara ili kugundua saratani mapema. Alisisitiza kuwa saratani si hukumu ya kifo iwapo itabainika mapema na mgonjwa kupata matibabu sahihi. Rais Samia alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa Jengo la Tiba ya Mionzi kwa Wagonjwa wa Saratani katika Kilimanjaro Christian Medical Centre, akionyesha kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika sekta ya afya.
