
Wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kushiriki katika mwelekeo mpya wa maendeleo ya Kiswahili ulioanzishwa na Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (KAKAMA). Mwelekeo huo utaanzishwa rasmi katika Kongamano la Kimataifa la Tatu linalofanyika Bujumbura, Burundi, kuanzia Julai 5, 2026, na kuambatana na maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani Julai 7.
