
Wakazi na wageni wa Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (DITF) wanapata huduma za kibenki ndani ya Viwanja vya Saba Saba kupitia Tawi la NMB Saba Saba, linalofanya kazi kuanzia Juni 28 hadi Julai 13, 2026. Tawi hilo linatoa huduma mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti, kuweka na kutoa fedha, malipo ya Serikali, bima, na huduma za kidijitali. Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, William Nkuna, alisema lengo ni kusogeza huduma karibu na wananchi na wafanyabiashara.